Wednesday 27 July 2016

Askari aliyepatikana na hatia ya kumuua mwandishi Daudi Mwangosi bila kukusudia, amehukumiwa miaka 15 jela

Leo July 27 2016 Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Iringa imetoa hukumu ya kesi ya mauaji ya aliyekuwa mwanahabari wa kituo cha Television cha chanel Ten, Daud Mwangosi.

Mahakama hiyo imemuhukumu kwenda jela miaka 15 mshtakiwa wa mauaji hayo, askari wa polisi kikosi cha kutuliza ghasia ‘FFU’ Pacificius Simon.

Hukumu hiyo imekuja baada ya juzi mahakama hiyo kumkuta na hatia askari huyo ya mauaji ya bila kukusudia ya Mwangosi yaliyofanyika September 2 2012 kwenye kijiji cha Nyololo, Mufindi  wakatia CHADEMA ikifanya uzinduzi  wa matawi, huku kukiwa na katazo la mikutano au makusanyiko ya kisiasa kutokana na seriakali kuongeza muda wa sensa ya watu na makazi

No comments: