Wednesday 17 August 2016

MGOGORO WA KANISA LA FREE PENTECOSTAL CHURCH MBEYA WACHUKUA SURA MPYA

Mgogoro wa kanisa la Free Pentecostal church lililopo forest ya zamani Mbeya, mjane wa mchungaji atolewa vyombo vyake nnje 

Mgogoro wa makanisa ya Free Pentecostal na Mbeya Pentecostal church kugombea aridhi pamoja na majengo umechukua sura Mpya baada Baraza la aridhi na nyumba kutoa agizo kuwa kanisa la Free Pentecostal church waondolewe kwenye majengo ya kanisa hilo na Mbeya Pentecostal church wakabidhiwe.

   Katika zoezi la kuondolewa kwa vyombo ndani ya majengo ya kanisa hilo,vilio vilitawala wakati zoezi limehamia kwenye nyumba ya mchungaji kutokana na hiyo nyumba kukaliwa na Mjane wa mchungaji. 

   Askofu wa Mbeya Pentecostal church Lamson Sikazwe amesema mgogoro huo ulianza mwaka 1998 ukaisha kisha ukaibuka tena mwaka 2002 hadi Leo ambapo wamepewa kibali na mahakama cha kuwaondoà Free Pentecostal church

No comments: