Thursday 24 August 2017

Majaliwa awakaribisha wafanyabiashara kutoka Cuba

SeeBait
Serikali imewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Cuba waje kuwekeza kwakuwa kuna fursa nyingi hapa Tanzania na kama zitatumika vizuri basi zitawezesha uchumi kuendelea kukua kwa kasi.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Havana nchini Cuba mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba, Lucas Domingo Polledo, ambapo amewakaribisha wafanyabiashara wa Cuba kuja kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya dawa.

Amesema kwa sasa Serikali ya Tanzania inaagiza dawa kutoka nje ya nchi jambo ambalo linasababisha kutumia fedha nyingi, hivyo uwepo wa kiwanda utasaidia katika kupunguza gharama.

Majaliwa ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda nchini kama mkakati wa kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati,


No comments: