Mwenyekiti wa mtaa wa akimsaidia kujaza
fomu ya kitambulisho cha Taifa mmoja wa wananchi waliojitokeza kusajiliwa
katika zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa wilayani Kyela mkoani Mbeya.
Usajili
Vitambulisho vya Taifa Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya umeanza katika Kata
za Matema, Makwale, Mababu na Ndobo na unatarajiwa kumalizika Jumamosi
Octoba 14, 2017 na kuendelea Kata zingine.
Ameeleza
faida za Mfumo wa Utambuzi na Usajili wa watu kwa Taifa na namna kila
mwananchi atakavyonufaika na mfumo huo utakapoanza kutumika na hivyo
kutoa wito kwa jamii hususani wananchi wa Wilaya ya Kyela kuhakikisha
wanajitokeza kwa wingi kusajiliwa.
Zoezi
la Usajili Vitambulisho vya Taifa limeanza kwa kishindo mikoa ya Kanda
ya Ziwa na Kaskazini na linakusudiwa kumalizika ndani ya muda mfupi
kutoa fursa kwa mikao mingine ya Tanzania kusajiliwa.
Mmoja wa wakaazi wa Mbeya akiweka saini ya
kielektroniki wakati wa zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa linaloendelea
wilayani Kyela.
Baadhi ya wananchi wakisubiri kusajiliwa
wakati wa zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa wilayani Kyela, wakati
wengine wakiendelea Kusajiliwa na Maafisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho
vya Taifa wakati zoezi linaendelea.
Wakazi
wa kijiji cha Kisyosyo Kata ya Matema wilayani Kyela mkoa wa Mbeya
wakichukuliwa alama za vidole wakati wa zoezi la Usajili wa Vitambulisho
vya Taifa katika mkoa wa Mbeya.
No comments:
Post a Comment