Tuesday 13 March 2018

Serikali ya Nigeria yatamani kufanya mazungumzo na Boko Haram


Serikali ya Nigeria imesema ina mpango wa kutumia njia ya mazungumzo badala ya kutumia nguvu za kijeshi ili kuwaokoa wasichana 110 waliotekwa katika mji wa Daptch hivi karibuni pamoja na wale waliotekwa mjini Chibok mwaka 2014.

Ofisi ya Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari imesema ingependa kuwapata wasichana waliotekwa Chibok na Daptch wakiwa hai.

Utekaji huo ndio mkubwa zaidi kufanywa na kundi la wanamgambo la Boko Haram lenye itikadi kali ya Jihadi, tangu lilipowateka wasichana wa shule 270 katika mji wa chibok mwaka 2014.

Hata hivyo, taarifa iliyowahi kutolewa na vyombo vya habari vya kiusalama ilidai kuwa takribani wasichana 100 waliachiliwa huru na Boko Haram baada ya kulipwa fidia na serikali.

No comments: