Saturday 18 April 2015

Boko Haram washambulia Cameroon, 10 wauawa



Boko Haram washambulia Cameroon, 10 wauawa

Wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram nchini Nigeria, wameshambulia vijiji vya kaskazini mwa Cameroon na kuua watu wasiopungua 10 na wengine kadhaa kujeruhiwa.

 Watu walioshuhudia wanasema kuwa, wanachama wa kundi hilo walitekeleza kwa pamoja hujuma hiyo asubuhi ya siku ya Ijumaa dhidi ya vijiji vya Biya na Bolabari katika eneo la Kolowata kaskazini mwa nchi hiyo.

 Inaelezwa kuwa, wanachama wa kundi hilo la kitakfiri walikimbilia Nigeria kupitia mpaka wa pamoja, baada ya majeshi ya serikali ya Cameroon kuwasili eneo la tukio.

 Nigeria ndio makao makuu ya kundi la Boko Haram, hata hivyo wanachama wake wamekuwa wakivuka mipaka ya nchi hiyo na kushambulia nchi za jirani, suala lililozipelekea nchi hizo kuunda kikosi cha pamoja kwa ajili ya kuendesha operesheni kali dhidi ya kundi hilo, operesheni ambazo zinatajwa kupata mafanikio makubwa hadi sasa.

No comments: