Wednesday 13 May 2015

HOSPITALI YA RUFAA MANYARA YAILALAMIKIA MSD KWA KUCHELEWESHA DAWA


Wauguzi katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Manyara pamoja na uongozi wa hospitali hiyo wameitaka idara ya boharia ya dawa nchini (MSD) kuondoa urasimu wa ucheleweshwaji wa manunuzi ya dawa na vifaa tiba ili kuepuka wagonjwa kubaki wodini kwa muda mrefu wakisubiri matibabu na pia urasimu huo husababisha vifo vinavyochangiwa na ukosefu wa dawa kwa wakati.

Kauli hiyo imetolewa kwenye maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani katika sherehe zilizofanyika kwa maandamano ya wauguzi wa hospitali hiyo kama kumbukumbu ya muasisi wa shughuli za uuguzi duniani Bi Florence Nightngale aliyezaliwa mei 12 1820 nchini Italia, huku mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dr Manyama Deogratius akitolea ufafanuzi wa changamoto za hospitali hiyo kukabiliwa na dawa na vifaa tiba kuwa husababishwa na mlolongo mrefu katika idara ya boharia unaochukua siku 14 hadi mwezi na kuitaka MSD kukiri ikiwa hawana dawa na ngazi ya mkoa itoe kipaumbele kwa upatikanaji wadawa kwa haraka.
 
Awali katika risala ya wauguzi wa hospitali hiyo kwa afisa masuhuri (katibu tawala mkoa) wamemueleza bayana kuwa licha ya hospitali hiyo kuanza kutoa huduma yake 2013 inakabiliwa na upungufu wa majengo na kutokamilika, pamoja na kuwepo kwa wauguzi 68,lakini ongezeko hilo halikidhi mahitaji kutokana na kuongezeka kwa huduma na kasi ya wagonjwa wasiopata huduma ya tiba.
Kwa upande wake kaimu afisa masuhuri (katibu tawala mkoa Manyara Bw Masaile Mussa licha ya kusisitiza nidhamu kwa wagonjwa na kukemea vitendo vya rushwa na ukatili kwa wauguzi bila ya kukiuka kiapo, lakini akisisitiza serikali kutambua changamoto zilizopo zikiwemo za zikiwepo za kuongeza wauguzi na kupandisha madaraja.
 
Kauli mbiu katika maadhimisho ya wauguzi mwaka huu yaa kumuenzi Muasisi Bi Florence Nightngale-wauguzi nguvu ya mabadiliko, huduma fanisi na gharama nafuu.
 

No comments: