Tuesday 19 May 2015

Viongozi na watanzania watakiwa kuienzi amani iliyopo ili wasije ingiza nchi vitani.


Viongozi wa Afrika wameaswa kuhakisha kuwa wanaweka mbali uchu wa madaraka ili wasiji kuzidumbukiza nchi zao katika vita na migogoro kama inavyotokea huko nchini Burundi huku watanzania wakitakiwa  kutambua kuwa amani iliyopo nchini ni lazima itunzwe na kamwe wasidanganyike kuwa hali ya amani iliyopo itaendelea kuwepo kama  wataligawa taifa katika misingi ya ukabila na udini.
Hayo yamesemwa na aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa nchi huru za Afrika Dk Salim Ahmed Salim na ambaye ni mwenyekiti wa taasisi ya Mwalimu Nyerere wakati akifungua mkutano wa mashauriano kuhusu  amani na umoja wa nchi, mkutano uliohusisha viongozi wa dini, wazee, siasa na wale wa vyama vya siasa.
Akizungumzia malengo ya mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na mwenyekiti mtendaji wa makammpuni ya IPP Dk Reginald Mengi pamoja na makamu wa kwanza wa rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, mkurugenzi wa taasisi ya Mwalimu Nyerere Mh Joseph Butiku amesema wameona ni busara kukaa na kuona nini kifanyike kuinusuru amani ya nchi hii hasa katika kipindi hiki ambacho inaonekana dalili za upotevu wa amani zimeanza kuonekana waziwazi.
Akitoa salamu za wazee Brigedia Jenerali Fransis Mbena amesma ili amebani iwepo lakixia wazee wa zamani na wa sasa watote wapewe hakili sawa na siyio kubagua kwania kwa kufanya hivyo ni kudhofisha misingi ya mani iliyopo.
Mkutano  pia ulihudhuriwa na wenyeviti wa vyama vya siasa akiwemo Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF na mwenyekiti wa NCCR mageuzi James Mbatia na pamoja na katibu mkuu wa Chadema Dk Wilbrod Slaa ambapo wamesema serikali inapaswa kuweka wazi ratiba ya uchaguzi ili kuepusha uvunjifu wa amani.

No comments: