Tuesday 21 July 2015

Mbunge wa Kahama Kupitia CCM, James Lembeli Atangaza Kujivua uanachama wa CCM na kujiunga na CHADEMA


2015 ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu Tanzania, kila siku stori za Siasa zimekuwa kwenye headlines nyingi kuanzia Magazetini, kwenye TV,  mitandaoni  na Radioni .

Mbunge James Lembeli alikuwa pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Mazingira na Maliasili.. kuna habari za baadhi ya Wabunge wametangazwa kuhama Vyama vyao, Lembeli kathibitisha kuhama CCM kwa maneno yake mwenyewe.

"Nimetafakari, nimezungumza na mama yangu kwa zaidi ya saa kumi.. mke wangu na watoto wangu, na kwa kusikia kilio cha wananchi wa Jimbo la zamani la Kahama nimeamua kutangaza kuanzia leo kwamba natangaza kujiondoa uanachama wangu ndani ya CCM" - James Lembeli.

"Nilikipenda lakini nimelazimika kuchukua uamuzi huu, najua nawakera wengi lakini nawaomba waangalie hali ambayo Viongozi wa CCM Wilaya ya Kahama wamesababisha niamue uamuzi huu mgumu.

"Kuanzia leo najiunga na CHADEMA… Namshukuru Rais Kikwete, nafikiri atakuwa mtu wa kwanza kuamini haya ninayosema, mwaka 2010 mizengwe iliyofanyika lengo lake ilikuwa kukata jina langu, kila mtu anafahamu Rais mwenyewe aliwahi kuniambia lakini Rais Kikwete ndiye aliyerudisha jina langu… Ninaahidi nitaendelea kufanya kazi nae mahali popote, na MUNGU naomba anisaidie niweze kuvuka salama katika haya"- James Lembeli.

No comments: