Sunday 5 July 2015

Rais kikwete awaonya baadhi ya viongozi wa dini kuacha kuwabeba baadhi ya wagombea.


Rais wa jamhuri wa Tanzania Mheshimiwa Dr,Jakaya Mrisho Kikwete amewaonya baadhi ya viongozi wa dini nchini ambao wamekuwa na viashiria vya itikadi za vyama vya siasa kuacha kuwabeba baadhi ya wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi ikiwemo ya urais na wabunge kwa sababu inaweza kusababisha choko choko za uvunjifu wa amani nchini.
Mheshiwa Rais Kikwete ametoa rai hiyo wakati wa sherehe za maadhimisho ya Jubilee ya miaka 125 ya kanisa la kiinjili la kilutheri nchini (KKKT) dayosisi ya kaskazini mashariki zilizofanyika katika viwanja vya mbuyu kenda jijini Tanga na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi, viongozi wa madhehebu ya dini pamoja na wageni kutoka taifa la Ujerumani ambao ndio waanzilishi wa dhehebu hilo nchini.
 
Awali akizungumza na maelfu ya waumini wa madhehebu tofauti wa ndani na nje ya nchi, askofu wa kanisa la kilutheri nchini dayosisi ya kaskazini mashariki Dr Stephen Munga amemuomba mheshimiwa rais kuhakikisha kuwa kipindi hiki cha uchaguzi mkuu ujao, nchi inaimarika kwa kuwa na amani kwa sababu yeye ndiye mwenye mamlaka makubwa ya kufikia malengo hayo kupitia chama chake.
 
Kufuatia hatua hiyo askofu mstaafu wa dayosisi ya kaskazini mashariki Joseph Jali amekemea viongozi wanaowabeba baadhi ya wagombea na kuonya kuwa rais hawezi kupatikana kwa njia ya nguvu zakibinadamu na badala yake mwenyezi mungu ndiye anayejua kuwa Tanzania itaongozwa na mtu atakayekuwa chaguo lake.
 

No comments: