Sunday 5 July 2015

Watanzania wana haki ya kuwezeshwa tena kwa upendeleo ili watumie fursa kujikwamua kiuchumi.


Watanzania wana haki ya kuwezeshwa tena kwa upendeleo maalum ili watumie fursa zilizopo na uwepo wa utajiri wa raslimali za asili kujikwamua kiuchumi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta binafsi nchini TPSF Dr Reginald Mengi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati Viongozi wa taifa na wa mikoa wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania JWT walipokutana na viongozi wa TPSF kujadili changamoto mbalimbali za biashara.
 
Amessma licha ya kuaminishwa kwa muda mrefu kuwa Tanzania ni nchi maskini, lakini kama nchi Tanzania ina ujajiri mkubwa wa raslimali, isipokuwa wananchi wake ndio maskini wanaohitaji serikali iwawezeshe ili waweze kutumia fursa na raslimali hizo kujikwamua kiuchumi.
 
Wakati wa mkutano huo uliohudhuriwa pia na baadhi ya wanachama wa JWT, waliazimia kuanzisha benki ya Wafanyabiashara baada ya kujiridhisha kuwa benki zilizopo si rafiki kwao.
Aidha viongozi hao walijadili kwa kina kuhusu kuwaruhusu wachuuzi wa kigeni kufanya biashara nchini zinazoweza kufanywa na watanzania, na mpango wa serikali wa kutaka kuwapatia Wachina eneo la Kurasini ili wajenge na kuendesha soko la kimataifa la bidhaa za viwandani, ambapo wameitaka serikali isitishe mpango huo na kulikabidhi eneo hilo kwa Watanzania ili kulinda biashara za Watanzania na uchumi wa Taifa.
 
Pia Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye ameishauri serikali kuuweka wazi mkataba wa kuliendeleza eneo hilo la biashara ili ifahamike nafasi na ushiriki wa wafanyabiashara wa Tanzania, huku Mwenyekiti wa taifa wa JWT Bw. Johnson Minja akisema mkutano huo ni hatua muhimu kwa maslahi na maendeleo ya wafanyabiashara nchini.
Wanachama wa JWT walimzawadia Dr Mengi sampuli chache za bidhaa wanazozitengeneza nje ha nchi kwa nembo zao binafsi za biashara na kuziuza hapa nchini.
 

No comments: