Wednesday 1 July 2015

Watu 4 wafariki na wengine 25 wajeruhiwa katika ajali ya Bus na Treni, Morogoro.


Watu 4 wamefariki dunia papo hapo na wengine 25 kujeruhiwa vibaya baada basi laabiria kampuni ya badcard likitokea Kilosa kwenda Morogoro kugonga Treni ya mizigo ikitokea Morogoro kwenda Dodoma katika eneo la kibaoni wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro ACP Mussa Marambo amefika katika eneo la tukio na kuthibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa gari kutokuwa mwangalifu wakati akivuka reli na nakuwataka madereva kuwa makini na kuzingatia sheria wanapo vuka katika makutano ya reli na barabara ili kuepusha ajali zisizokuwa za lazima zinazogharimu maisha ya watu.
 
Kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kilosa Dk Denis Haule amekiri kupokea maiti 4 pamoja na majeruhi 25 ambapo kati yao watano hali zao ni mbaya nawamehamishiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi ambapo katika hatua nyingine amelalamikia shirika la umeme Tanzania Tanesco kuweka umeme wa luku katika hospitali ambapo wakatiwa tukio la ajali imesababisha kero kubwa na kushindwa kuwahudumia majeruhi kwa wakati na kulazimika kuchukua muda mrefu kutafuta jenereta.
 
Nao majeruhi na mashuhudia watukio hilo wameeleza jinsi tukio lilivyotokea ambapo wametupia lawama dereva wa treni kutopiga honi kwa tahadhari na kusababisha  ajali ambayo imegharimu maisha ya watu kwa kusabsiha vifo, na vilema vya kudumu kwa abira wasiokuwa nahatia.
 
Katika tukio hilo waliofariki ni mwanamke mmoja, wanaume wawili pamoja mtoto mdogo na kati ya majeruhi 25 watano kati yao ni watoto wadogo na wanaendlea na matibabu katika hospitali ya wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro

No comments: