Tuesday 9 May 2017

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 08.05.2017.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA


 
                                                                                                              Ofisi ya Kamanda wa Polisi,                                                                                                                                                                                                                                                                                                   Mkoa  wa  Mbeya,                                                                                    
Namba ya simu 2502572                                                                                               S. L. P. 260,
Fax - +255252503734                                                                                                       MBEYA.
              tanpol.mbeya@gmail.com
                                                       
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 08.05.2017.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu.


KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI

Mnamo tarehe 06.05.2017 majira ya saa 21:30 usiku huko katika Kijiji cha Mahongole, Kata ya Imalilo - Songwe, Tarafa ya Rujewa, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Polisi lilifanya msako na kufanikiwa kumkamata mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la MARIAM SIMON [25] Mkazi wa Mahongole akiwa na vipande 19 vya nyama ya ngiri katika nyumba yake.

Mtuhumiwa alikamatwa na nyama hizo baada ya kupekuliwa katika nyumba yake anayoishi pamoja na mumuwe ambaye amefanikiwa kukimbia. Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo. Upelelezi unaendelea.

KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.

Mnamo tarehe 07.05.2017 majira ya saa 13:00 mchana huko maeneo ya Forest, Kata ya Forest, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Polisi lilifanikiwa kumkamata mtu mmoja aitwaye CALVIN SHILONGI @ MAHEMBE [24] raia na mkazi wa nchini Botswana kwa kosa la kuingia nchini bila kibali. Upelellelzi unaendelea.


Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaongeza jitihada kwa kushirikiana na wadau wengine wa usalama katika kuzuia na kupunguza ajali za barabarani kwa kuhakikisha madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatii, wanaheshimu na kufuata sheria za usalama barabarani. Aidha kumekuwa na tukio 01 la ajali ya kifo kama ifuatavyo:-




Mnamo tarehe 08.05.2017 majira ya saa 05:10 Alfajiri huko eneo la Sokoine, Kata na Tarafa ya Sisimba, Jijini Mbeya katika Barabara ya Mafiati-Sokomatola, Gari yenye namba za usajili T.866 CGC aina ya Toyota Honda iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aitwaye FRANK MWAISANILA umri kati ya miaka 25 - 30 Mkazi wa Isyesye iliacha njia, kupinduka na kusababisha kifo kwa dereva huyo.

Aidha katika ajali hiyo mtu mmoja ambaye alikuwa abiria katika gari hiyo aitwaye JOHN CHOGO [28] Mkazi wa Sokomatola alijeruhiwa na kupelekwa Hospitali ya Rufaa Mbeya ambapo alipatiwa matibabu na kuruhusiwa.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Mbeya.


WITO:

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za siri kwa Jeshi la Polisi ili ziweze kufanyiwa kazi kwa haraka. Pia Kamanda KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kuwa makini na watu wanaowatilia mashaka hasa wahamiaji haramu kwa kutoa taarifa mapema ili upelelezi dhidi yao ufanyike.

            Imesainiwa na:
                            [DHAHIRI A. KIDAVASHARI - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA


No comments: