Monday 18 September 2017

Peter Msigwa: Sitaki Kuviziwa, Wakinihitaji kwa Utaratibu Maalumu Ntaitikia Wito


SeeBait
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kusema kuwa amepata taarifa jeshi la polisi linamtafuta na kusema endapo jeshi la polisi litamwita kwa kufuata utaratibu basi na yeye ataitika wito huo ila si kuviziwa

Mbunge Msigwa ametoa taarifa hii kufuatia kuwepo kwa taarifa toka jana kuwa kiongozi huyo naye anatafutwa na jeshi la polisi akidai kuwa ni moja kati ya watu waliokuwa wakiratibu mkusanyiko wa maombi ambao ulitakiwa kufanyika jana kumuombea Mbunge Tundu Lissu katika viwanja vya TIP Sinza jambo ambalo yeye mwenyewe alipinga na kusema bado yupo nchini Kenya.

"Nimepata taarifa Kuwa polisi wamenitafuta toka asubuhi (jana) maeneo ya sinza, Wakisisitiza kuwa nipo hotelini hapo , wakati mimi niko Nairobi, nitaitika wito wa polisi ukiletwa rasmi, sihitaji kuviziwa +255754360996 mnaweza kunipigia au kunitumia ujumbe mfupi Whatsaap" alisema Msigwa.

Mbunge Peter Msigwa bado yupo jijini Nairobi nchini Kenya kwenye matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambaye alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

No comments: