Saturday 27 June 2015

Serikali yaja na mpango wa usimamizi wa raslimali za maji bonde la Rufiji.



Kutoshirikishwa kikamilifu kwa wadau na watumiaji wa rasilimali za maji nchini kumedaiwa kuwa ndiyo chanzo cha migogoro mingi ya watumiaji maji ikiwa ni pamoja na athali mbalimbali zinazosababisha kupungua kwa rasilimali hiyo na kukauka kwa baadhi ya mito.
Hayo yamesemwa na mkuregenzi msaidizi wa raslimali za maji kutoka wizara ya maji Dokta George Lugomela wakati akizungumza mjini iringa na wadau wa usimamizi wa raslimali za maji kwenye bonde la rufiji linalijumuisha mikoa 11 nchini na kueleza kuwa kwa muuda mrefu serikali haikuwa na mpango madhubuti unaosimamia raslimali za maji hali iliyopelekea migogoro mingi na hata matumizi yasiyo endelevu.
 
Afisa wa maji bonde la rufiji Idris Msuya amese bonde hilo licha ya kuwa na mabwawa ya kuzalisha umeme ya mtera na kidatu pia ni maarufu kwa kilimo kutokana na kuwa na hali ya hewa inayostawisha mimea mbalimbali na hivyo kuwa eneo muhimu kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo hivyo uwepo wa raslimali hizo unahitaji mpango mahususi wa usimamizi wa maji katika bonde hilo lenye ukubwa wa karibu kilometa za mraba laki mbili.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya kilolo Seleman Mzee aliyemwakilisha mkuu wa mkoa wa iringa katika mkutano huo wa wadau wa maji uliolenga kujadili mpango wa usimamizi na uendelezaji raslimali za maji ulioandaliwa na serikali kwa kipindi cha miaka mitano na kughalimu kiasi cha dola bilioni moja nukta tano amesema mpango huo utaondoa matumizi ya maji yasiyofuata utaratibu huku mwaandaaji wa mpango huo Profesa Alice Georgakakos akisema kuwa mpango huo pamoja na mambo mengine pia umeainisha changamoto na fursa zilizopo katika matumizi ya raslimali za maji katika eneo husika.

No comments: