Friday 30 September 2016

KAZI IMEANZA, HILI NDIYO JOTO LA WATANI WA JADI, YANGA NA SIMBA


Watani wa jadi, Yanga Vs Simba wanakutaka kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Lakini joto la mechi hiyo linazidi kupanda kwa kasi kubwa, hasa mitaani kwa watu kuvaa mavazi yanayoashiria wanasapoti timu gani.

Mfano, gari hilo aina ya VW ‘Bito’, mwenyewe anaonyesha kabisa ni shabiki wa Yanga au Wanajangwani na anajiamini kwamba, kesho wao ni kama kawa.

No comments: