Wednesday 20 September 2017

Mbunge Kubenea ashindwa kuhojiwa na kamati ya Bunge


Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amepelekwa katika zahanati ya Bunge baada ya kujihisi vibaya.
Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema leo Jumatano kuwa, Kubenea amefika mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na amewaeleza kwamba hali yake si nzuri.
Kutokana na hilo, amesema amepelekwa kwenye zahanati hiyo na hali yake itakapoimarika atahojiwa na kamati.
Mbunge huyo ambaye alipelekwa Dodoma kwa ndege leo asubuhi, jana Jumanne alisema alikuwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay  wilayani Kinondoni akisubiri utaratibu wa safari hiyo ya kwenda kuhojiwa kama Spika wa Bunge Job Ndugai alivyoagiza.

No comments: